“Kuna zaidi ya wanafunzi 16,000 ambao hawatapata fursa ya
kujiunga na chuo kikuu mwaka huu, kulingana na mwongozo wa sasa kwamba
waliopata alama mbili wasidahiliwe,” alisema Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Baamoyo,
Profesa Costa Mahalu na kuongeza:
“Hiki ni kiama kwa vyuo vikuu binafsi, maana idadi ya
waliopata alama nne ni ndogo na inawezekana wote wakaenda kwenye vyuo vikuu vya
umma. Kibaya zaidi hakuna mahala ambako Serikali imepanga kuwapeleka hao ambao
hawatadahiliwa.”
Kauli ya Profesa Mahalu iliungwa mkono na wahadhiri
wengine kadhaa, waliosema kuwa kitendo cha Serikali kupandisha alama ya ufaulu
wa kujiunga na chuo kikuu, kitaongeza ‘vilaza’ badala ya kuwapunguza.
Mmoja wa wahadhili hao kutoka Chuo Kikuu cha Sayansi ya
Tiba (IMTU), ambaye hakutaka kutajwa gazetini kwa kile alichoeleza kuwa si
msemaji wa chuo, alisema: “Mtu hawezi kuwa ‘kilaza’ akiwa chuo kikuu.”
Facebook Blogger Plugin by Tanzaniastar
Post a Comment