Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
HATUA ya Serikali ya kupandisha kiwango cha ufaulu wa kujiunga na chuo kikuu kutoka alama mbili hadi nne, itavifanya vyuo vikuu binafsi vikose wanafunzi katika mwaka wa masomo 2016/17, JAMBOLEO limeelezwa. Habari kutoka baadhi ya vyuo hivyo, ikiwamo vilivyofungwa kudahili wanafunzi mwaka huu, imeeleza kuwa uamuzi huo wa Serikali utawaondoa kwenye udahili wanafunzi 16,000 waliopata alama mbili katika matokeo ya kidato cha sita yaliyotangazwa hivi karibuni.

“Kuna zaidi ya wanafunzi 16,000 ambao hawatapata fursa ya kujiunga na chuo kikuu mwaka huu, kulingana na mwongozo wa sasa kwamba waliopata alama mbili wasidahiliwe,” alisema Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Baamoyo, Profesa Costa Mahalu na kuongeza:
“Hiki ni kiama kwa vyuo vikuu binafsi, maana idadi ya waliopata alama nne ni ndogo na inawezekana wote wakaenda kwenye vyuo vikuu vya umma. Kibaya zaidi hakuna mahala ambako Serikali imepanga kuwapeleka hao ambao hawatadahiliwa.”
Kauli ya Profesa Mahalu iliungwa mkono na wahadhiri wengine kadhaa, waliosema kuwa kitendo cha Serikali kupandisha alama ya ufaulu wa kujiunga na chuo kikuu, kitaongeza ‘vilaza’ badala ya kuwapunguza.
Mmoja wa wahadhili hao kutoka Chuo Kikuu cha Sayansi ya Tiba (IMTU), ambaye hakutaka kutajwa gazetini kwa kile alichoeleza kuwa si msemaji wa chuo, alisema: “Mtu hawezi kuwa ‘kilaza’ akiwa chuo kikuu.”

Thanks For Visiting, Our Website Come Again For News, Advertisement And Good Articles

Keep This blog site In Your Mobile For More Updates

Facebook Blogger Plugin by Tanzaniastar
https://www.facebook.com/Tanzaniastar
Next
Newer Post
Previous
This is the last post.

Post a Comment

 
Top