Kwa mujibu wa Polisi, majambazi hao walikuwa wakiwaongoza kuelekea walikojificha wenzao wanaodaiwa kuhusika na tukio la wizi kwenye tawi la CRDB Mbande, wilayani Temeke na mapigano na polisi hivi karibuni Vikindu.
Mmoja wa majambazi hao akiwa ni raia wa Kenya, wamehusika na tukio lililotokea hivi karibuni na askari wanne kuuawa na wanaodaiwa kuwa ni majambazi kupora silaha na kukimbilia msitu wa Vikindu, Mkuranga.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Simon Sirro alisema Jeshi lake limekamata majambazi zaidi ya saba mmoja akiwa raia wa Kenya, kati ya zaidi ya 14 waliohusika na tukio la Vikindu na kumwua Ofisa wa Polisi Mwandamizi.
Alisema Jeshi hilo limekamata mtandao wa majambazi watatu ambao walipatikana wakiwa na silaha 23 na risasi 835.
Facebook Blogger Plugin by Tanzaniastar







Post a Comment